RADIO BEROYA FM

vendredi, février 6News That Matters
Shadow

Poutine akemea “histeria ya Ulaya” na kukataa uvumi wa shambulio la Urusi

Katika hotuba yake kwa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, Vladimir Poutine amekashifu madai ya uwezekano wa mashambulizi dhidi ya Ulaya. Rais wa Urusi ameyaita “uongo na upuuzi” na kuwatuhumu viongozi wa Ulaya kwa kuchochea hofu bandia. 

Rais Vladimir Poutine ameyapinga kwa msimamo thabiti madai kwamba Moscow inapanga shambulio dhidi ya Ulaya.

Akizungumza Jumatano katika kikao kilichopanuliwa cha baraza la Wizara ya Ulinzi, aliyaeleza madai hayo kuwa ni “uongo na upuuzi.”

Kwa mujibu wake, viongozi wa kisiasa wa Ulaya wanatafuta kuchochea histeria na kupanda mbegu za hofu katika fikra za wananchi.

“Viongozi wa kisiasa wa Ulaya wanachochea histeria na kupanda hofu kuhusu dhana ya kutokwepeka kwa makabiliano na Urusi,” alisema Vladimir Poutine, akikaririwa na Russia Today (RT).

Kiongozi wa Kremlin anaona kuwa hotuba hizi za kutisha zinakusudia kuhalalisha siasa za makabiliano na kuimarisha ujeshi wa bara hilo.

Amesisitiza kwamba Urusi haijawahi kutangaza nia ya uvamizi dhidi ya majirani zake, huku akibainisha kuwa itaendelea kuwa makini mbele ya vitisho vinavyoonekana katika mipaka yake.

Kauli hii imetolewa katika mazingira ya mvutano unaoendelea kati ya Moscow na Magharibi, mvutano unaojitokeza kupitia tofauti za mtazamo kuhusu usalama wa Ulaya na migogoro ya kikanda.

Emmanuel Kasereka bin Vikingi

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *