RADIO BEROYA FM

lundi, mars 16News That Matters
Shadow

Marekani“America First, kwa nguvu zaidi: Trump avuruga mpangilio wa dunia”

Mwaka mmoja baada ya kurejea Ikulu ya White House, Donald Trump amethibitisha kwamba falsafa yake ya America First ndiyo injini ya utawala wake. Kupitia kufukuza wahamiaji kwa wingi, vita vya kibiashara na kujiondoa kutoka mashirika ya kimataifa, Marekani inazidi kujitenga, ikidhoofisha ushirikiano wake na kuingiza dunia katika hali ya sintofahamu.  

Tarehe 20 Januari 2025, Trump alikamata tena hatamu za uongozi. Ndani ya siku chache tu, alitia sahihi misururu ya amri za urais, ishara ya mwendelezo wa sera zake za awali na azma ya kuvunja utaratibu wa ushirikiano wa kimataifa.

Sera ya uhamiaji imekuwa kali zaidi kwa kufukuza wahamiaji kwa maelfu, huku vita vya kibiashara vikiongezeka. Kodi za forodha dhidi ya China, India na Umoja wa Ulaya zimeweka msingi wa mvutano wa kiuchumi.

Trump ameendeleza misururu ya kujiondoa au kutishia kujiondoa Marekani kutoka mashirika kadhaa ya kimataifa. Mkakati huu wa upande mmoja unaonyesha kutoamini kwa kina taasisi za ushirikiano wa kimataifa na unazidisha upweke wa Marekani.

Mahusiano na Ujerumani yamezorota, hasa kutokana na vitisho kuhusu Greenland na lawama dhidi ya NATO. Ulaya, ambayo zamani ilikuwa mshirika wa karibu, sasa inatafuta kuimarisha uhuru wake wa kimkakati.

Mtindo huu unazidisha hali ya kutotabirika kwa Marekani na kuwalazimisha washirika wake kupanga upya ushirikiano wao. Asia na Ulaya zinachunguza ushirikiano mpya ili kupunguza utegemezi wao kwa Washington.

Kwa mujibu wa Foreign Policy, Trump anasababisha “madhara ya kudumu” kwa mpangilio wa dunia. Time Magazine inasisitiza mantiki ya vitisho vyake vya kiwango cha juu, ilhali Foreign Affairs inatoa tafsiri yenye matumaini zaidi, ikiona mkakati wake kama jaribio la “amani kwa nguvu.”

Akiwa na miaka mitatu mingine mbele yake, Trump anaendeleza sera ya mambo ya nje inayojengwa juu ya upande mmoja na mvutano. Wafuasi wake wanaiona kama urejesho wa nguvu za Marekani, lakini wachambuzi wengi wanakosoa mwelekeo wa kujitenga unaodhoofisha uwiano wa kimataifa.

Emmanuel Kasereka bin Vikingi

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *