Pamoja na Sant’Egidio, Goma yaipa sauti amani: Tuchague amani, tujenge umoja
Jumamosi tarehe 8 Novemba 2025, hoteli ya Cap Kivu mjini Goma iligeuka kuwa jukwaa la mkutano wa kipekee wa kidini uliohusu kaulimbiu Kuthubutu amani. Tukio hili lililoandaliwa na jumuiya ya Sant’Egidio liliwaleta pamoja viongozi wa dini mbalimbali—Waislamu, Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana—pamoja na vijana, watoto na wazee, wote wakiwa na azma ya kujenga mustakabali wa undugu na mshikamano.
Hotuba zilizotolewa zilisistiza umuhimu wa kugeuza wapinzani kuwa ndugu, kuweka mbele maslahi ya pamoja, na kutanguliza heshima ya utu wa binadamu. Amani ilielezwa kuwa ni nguvu ya kimungu, chaguo la maisha, na jukumu la kila mmoja kwa unyenyekevu na uendelevu.
Mtoto mmoja kutoka Sant’Egidio alitamka kwa msisimko: “Kuthubutu amani ni kuitaka amani, ni kuijenga amani, na ni kuishi amani.” U...







