Beni: Wakulima walalamikia unyanyasaji unaodaiwa kufanywa na Wazalendo huko Mikuha-Kididiwe
Wakulima wa maeneo ya Mikuha Kididiwe, iliyoko katika vijiji vya Bapakombe-Bakondo, wilaya ya Beni (Kivu Kaskazini), wamelalamikia vitendo vya unyanyasaji ambavyo wanavihusisha na wapiganaji wa Wazalendo wanaofanya shughuli katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa wakazi kadhaa waliowasiliana na mwana ripota wetu,wapiganaji hao waliwalazimisha wananchi siku ya Jumatatu, tarehe 9 Machi 2026, kufanya kazi za lazima ikiwemo kubeba mbao kwa ajili ya shughuli zao. Wakulima wanasema kwamba kazi hizo ziliwalazimishwa raia bila kujali umri, jambo lililoibua hasira katika jamii ya wenyeji.
Wananchi wanaona kwamba vitendo hivyo ni aina ya dhuluma dhidi ya watu ambao tayari wanakabiliwa na changamoto nyingi za kiusalama na kiuchumi. Wanasikitika kwamba hawa Wazalendo, ambao walitarajiwa kusaidia kulinda r...




