
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itachuana na Algeria Jumanne tarehe 6 Januari 2026 saa kumi na moja jioni (17h00 kwa saa za eneo) katika Uwanja wa Prince Moulay Hassan mjini Rabat, kwenye mchezo muhimu wa hatua ya mtoano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2025.
Mkutano huu unakutanisha timu mbili zenye ari na mwendo mzuri katika mashindano. Algeria, ikiwa haijapoteza mchezo wowote katika hatua ya makundi, ilimaliza kileleni mwa kundi lake kwa ushindi wa michezo mitatu mfululizo, ikionyesha uimara mkubwa wa safu ya ushambuliaji na ulinzi.
Kwa upande wake, DRC nayo ilikamilisha hatua ya makundi bila kupoteza, ikiwa na ushindi mara mbili na sare moja, ikitegemea kikosi kilichopangika vyema na chenye ufanisi katika mapambano.
Kwa Wacongo, huu ni mtihani wa kupiga hatua na kuendeleza safari ya kupendeza ya bara la Afrika. Kwa Waarabu wa Algeria, ni nafasi ya kuthibitisha hadhi yao ya kifavori na kufika robo fainali.
Romulus Nzalumbo