
Mwisho huu wa mwaka 2025, jiji la Butembo limegeuka kuwa jukwaa la sherehe kubwa ya kitamaduni: Kermesse ya Amani. Wasanii, harakati na wananchi wanakusanyika kuimba kwa sauti moja amani, undugu na kutokua na vurugu.
Kermesse ya Amani imefunguliwa Butembo sambamba na sherehe za mwisho wa mwaka. Tukio hili la kitamaduni linakusudia kuziunganisha jamii zote chini ya wazo moja: amani na undugu.
Miongoni mwa washiriki, harakati ya rasta Ouran imejitokeza kwa ujumbe wake wenye nguvu wa kuhimiza umoja wa Afrika na kurejea katika thamani za kitamaduni za Kibantu.
Mmoja wa viongozi wa harakati hiyo, alipoongea na vyombo vya habari, alisisitiza: “Lengo letu ni kufikisha ujumbe wa amani, ujumbe wa kutokua na vurugu.”
Harakati hiyo imehamasisha orkestra Afrikan Black Stone, ambayo itapamba sherehe kwa midundo ya reggae yenye matumaini na mshikamano.
Katika nafasi ya juu ya jukwaa, msanii Black Sadja 12 Poumons, anayejulikana kama mwana wa kifalme wa reggae Afrika ya Kati, anatarajiwa kutoa tamasha la kipekee tarehe 1 Januari 2026.
Shughuli zote zinafanyika katika Uwanja wa Tsaka Tsaka, mahali pa mkusanyiko ambapo wananchi na wasanii kadhaa wamealikwa kushiriki katika nyakati za undugu na sherehe.
Kwa wakati huu, harakati ya rasta Ouran imezindua Jumba la Umoja wa Mataifa ya Kibantu, baraza lililojengwa na wanachama wake, likiwa alama ya mazungumzo na mshikamano wa Kiafrika.
Emmanuel Kasereka bin Vikingi