RADIO BEROYA FM

lundi, mars 16News That Matters
Shadow

Afya ya Wanawake Goma: CIMAK yafungua milango kwa uchunguzi wa saratani ya matiti

Huko Goma, Kituo cha Afya New Deal / CIMAK kimepiga hatua muhimu katika mapambano dhidi ya saratani ya matiti. Tangu tarehe 18 Februari 2026, hospitali hii imeanzisha mpango wa kila siku wa uchunguzi kwa kutumia mammografia, ikiwakaribisha wanawake na wasichana kuchukua hatua za kulinda afya zao na kuzuia maendeleo ya kimya ya ugonjwa huu.  

Hospitali ya New Deal / CIMAK imetangaza rasmi kuanzishwa kwa mpango wa uchunguzi wa saratani ya matiti kwa wakazi wa Goma na maeneo ya jirani, kwa kuzingatia hasa wanawake na wasichana.

Saratani ya matiti bado ni miongoni mwa visababishi vikuu vya vifo vya wanawake duniani. Wataalamu wanakumbusha kwamba uchunguzi wa mapema huongeza kwa kiwango kikubwa nafasi ya matibabu yenye mafanikio na uponyaji. “Kujipima mapema ni kulinda maisha yako,” yasema uongozi wa hospitali.

Katika muktadha huu, idara ya picha za kitabibu ya CIMAK inafanya uchunguzi wa mammografia kila siku, ikiwapatia wagonjwa mazingira ya kitaalamu, salama na yenye usiri.

Lengo kuu ni kuwasaidia wanawake kufahamu hali ya afya ya matiti yao na kuzuia maendeleo ya kimya ya ugonjwa huu. Uongozi unasistiza umuhimu wa hatua hii: “Kujua hali ya matiti yako ni jambo la msingi katika kuzuia na kugundua mapema saratani ya matiti.”

Mpango huu ni mwito wa uwajibikaji wa wanawake na uangalizi wa kiafya. Wanawake na wasichana wa Goma wanahimizwa kutumia fursa hii ili kulinda afya zao.

Kwa maelezo zaidi, wahusika wanaweza kufika moja kwa moja hospitalini, iliyoko namba 43, Avenue de la Frontière, mtaa wa Commune de Goma, nyuma ya chuo cha Lac ex Kinyumba, au kuwasiliana kupitia namba hizi: +243 860406812 / +243 860406811.

Taarifa za ziada pia zinapatikana kupitia anuani za barua pepe: info@newdealcimak.org na info.cimak@gmail.com, pamoja na tovuti rasmi: www.newdealcimak.org.

Emmanuel kasereka Bin Vikingi

Laisser un commentaire

Votre adresse e-mail ne sera pas publiée. Les champs obligatoires sont indiqués avec *